Home Soka Mourinho Kocha Mpya Totts

Mourinho Kocha Mpya Totts

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Tottenham imemteua Jose Mourinho kuwa kocha mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Mauricio Pochetino ambaye amefukuzwa kutokana na matokeo mabaya kwa siku za hivi karibuni.

Mourinho (56) amesaini mkataba wa miaka mitatu ambao utadumu mpaka mwaka 2023 ili kuleta mataji klabuni hapo baada ya Pochetino kushindwa kuleta taji lolote tangu ateuliwe mwaka 2014 na kufanya timu hiyo kutochukua kombe lolote tangu mwaka 2008.

Pochettino amefukuzwa klabuni hapo baada ya kudumu kwa miaka mitano huku mtendaji mkuu wa klabu hiyo Daniel Levy alisema “kwa Mourinho tumepata meneja mwenye mafanikio duniani”.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited