Home Soka Mwakyembe Apigwa Chini

Mwakyembe Apigwa Chini

by Sports Leo
0 comments

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dr. Harison George Mwakyembe ameshindwa kwenye kura za maoni kuteuliwa kugombea Jimbo la Kyela Mbeya kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mwakyembe amekuwa Mshindi wa Tatu Baada ya kupata kura 252 huku Mshindi wa Pili Hanta Albert Mwakifuna akipata kura 288 na kwanza ni Ally Mlagila Jumbe (Kinanasi) (Mwenye suti nyeusi katikati) akipata kura 502.

Hata nafuu aliyonayo Waziri huyo wa michezo ni kusubiri Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi ambayo itakaa na kupitia majina ya washindi hao ili kuyapitisha ambapo pia mgombea aliyeshinda kura za maoni anaweza asipitishwe kusimamishwa kama mgombea wa chama.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited