Mashabiki wa klabu ya Simba Sc sasa mkae mkao wa kula baada ya mabosi wa klabu hiyo kupambana na kukamilisha usajili wa mshambuliaji hatari kutoka Tanzania, Selemani Mwalimu ambaye ametua kwa mkopo akitokea mabingwa wa Morocco, Wydad Athletic Club (WAC).
Habari hii imeleta msisimko mkubwa mitaani na mitandaoni, huku mashabiki wa Simba wakiamini ujio wa Mwalimu utakuwa silaha ya moto kwenye mbio za Ligi Kuu Bara na michuano ya kimataifa ya CAF Champions League.
Mwalimu, ambaye amewahi kuzichezea timu ya Singida Black Stars na Fountain Gate Fc za hapa nchini kisha kutua Wydad anatambulika kwa kasi yake ya kushambulia na uwezo wa kufumania nyavu ambapo amesaini dili la mkopo la msimu mzima wa 2025-2026 nafasi ya kuvaa jezi nyekundu kwa msimu huu.
Akizungumza baada ya kukamilisha usajili huo straika huyo alisema:
“Simba ni klabu kubwa, yenye historia na mashabiki wa aina yake. Nimekuja kuongeza nguvu na kuhakikisha tunafanikisha malengo ya kutwaa mataji makubwa. Najua presha ipo, lakini hii ndiyo nafasi yangu ya kuonyesha thamani yangu.”
Kwa upande wake, mmoja wa viongozi wa Simba SC amethibitisha kuwa Mwalimu atakuwa sehemu ya kikosi kitakachoanza maandalizi ya mechi ngumu zijazo wakianza na Ngao ya jamii dhidi ya Yanga sc kisha mechi za hatua ya awali ya Caf Champions League.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Tulihitaji kuongeza makali ya ushambuliaji na Mwalimu ni jibu sahihi. Ni kijana mwenye njaa ya mafanikio, na tunajua ataendana na falsafa ya kocha wetu Fadlu Davis ambaye alisema anahitaji mshambuliaji mwenye sifa ya X-Factors,” alisema kiongozi huyo.
Kwa mashabiki wa Msimbazi, huu ni ujio wa “mwana nyumbani” anayetarajiwa kuongeza kasi ya mashambulizi sambamba na washambuliaji waliopo.
Tayari mitandao ya kijamii ya klabu ya Simba Sc imefurika jumbe za kumkaribisha baada ya kutambulishwa rasmi kupitia kurasa hizo na mashabiki wakiahidi kujitokeza kwa wingi kumshuhudia akianza kucheza chini ya jezi nyekundu.
Simba SC msimu huu imejipanga kutwaa kila taji lililo mbele yao, sasa inaonekana kupeleka ujumbe kwa wapinzani wao wa jadi Yanga SC na wapinzani wa kimataifa kwamba safari ya Msimbazi msimu huu si ya masihara hasa baada ya kufanya sajili za maana kabisa.