Home Soka Namungo Yafunga Usajili na Kagere

Namungo Yafunga Usajili na Kagere

by Sports Leo
0 comments

Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Singida Fountain Gate Fc Meddie kagere amejiunga na klabu ya Namungo yenye maskani yake mkoani Mtwara katika wilaya ya Ruangwa kwa mkataba wa mkopo wa miezi 6.

Mchezaji huyo wa zamani wa Simba sc alijiunga na Singida Fountain Gate mwaka ambapo baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa nusu msimu sasa amejiunga na Namungo Fc kumalizia sehemu ya pili ya msimu huu wa ligi kuu na Nbc.

Pia klabu hiyo imemsajili Aliyewahi kuwa kiungo Vilabu vya Coastal Union na Mbeya City Fc Ayoub Semtawa kwa mkataba ambao haukuwekwa wazi na mabosi wa klabu hiyo yenye mashabiki wengi katika mikoa ya kusini mwa Tanzania.

banner

Katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc ambayo mpaka sasa imesimamishwa Namungo Fc inashika nafasi ya nane ikiwa na alama 17 ikiwa imecheza jumla ya michezo 14 mpaka sasa ambapo usajili wa Kagere unakwenda kuziba pengo la mshambuliaji Reliants Lusajo ambaye amejiunga na Mashujaa Fc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited