Home Soka Neymar Kuikosa Kopa America

Neymar Kuikosa Kopa America

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambualiaji wa Brazil Neymar Jr ataikosa michuano ya kombe la shirikisho barani America maarufu kama Kopa Amerika baada ya kuumia kifundo cha mguu wake wa kulia katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na michuano hiyo dhidi ya Qatar hapo jana.

Staa huyo anaichezea klabu ya Psg ya nchini Ufaransa aliumia dakika 20 za mwanzo wa mchezo baada ya staa wa Everton Richalson kuifungia Brazil bao la kwanza kwa kichwa na wakati wachezaji wenzie wakiungana kushangilia,Neymar alionekana akielekea vyumbani na timu ya madaktari kwa ajili ya matibabu na baadae aliondoka kabisa uwanjani hapo.

Nyota huyo hakuwa na msimu mzuri baada ya hivi karibuni kukosa mechi za 13 klabu yake sababu ya majeraha,Pia wiki iliyopita alitolewa unahodha wa timu ya taifa na nafasi yake alichukuliwa na mkongwe Dani Alves.

banner

Katika taarifa iliyotolewa na chama cha soka cha Brazil inasema mchezaji huyo atakosa michuano hiyo baada ya vipimo kuonesha amepata matatizo katika kifundo cha mguu hivyo hataweza kushiriki michuano hiyo huku benchi la ufundi la timu ya taifa litatafuta mchezaji atakayeziba nafasi ya staa huyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited