Home Soka Ngorongoro Mabingwa Chalenji

Ngorongoro Mabingwa Chalenji

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya vijana ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) imetwaa ubingwa wa michuano ya kombe la chalenji kwa vijana iliyofanyika nchini Uganda baada ya kuifunga Kenya kwa bao 1-0 katika fainali iliyomalizika jioni hii.

Ngorongoro ilipata goli hilo dakika ya 46 baada ya Otieno Onyango kujifunga na mpaka mechi inamalizika Heroes ilifanikiwa kulilinda bao hilo hivyo kuwafanya kutangazwa mabingwa wa michuano hiyo huku wakiweka rekodi ya kushinda mechi zote katika michuano hiyo.

Kelvin John alifanikiwa kuchukua tuzo ya mfungaji bora wa michuano hiyo baada ya kufunga mabao 7 na kuwazidi washambuliaji wote huku akipata pia tuzo ya mchezaji bora wa michuano hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited