Mshambuliaji wa Inter Milan Romelu Lukaku, amesema kuwa kwasasa ameimarika zaidi tangu alipo hamia Inter Milan kutoka Manchester United.
Akizungumza na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry kupitia Instagram Live, Lukaku alisema, anafanya kazi yake kwabidii kuhakikisha kuwa anakuwa bora zaidi.
Lukaku ambaye aliuzwa na united kwa takribani pauni Milioni 73 alimwambia Henry”Unapoimarika sio tu juu yako mwenyewe, kufunga magoli ndio dawa yangu, kitu ambacho kipo ndani ya moyo wangu. Lakini bado naendelea kujifunza. Nadhani nataka kuisaidia timu yangu, natakiwa kuwa nauwezo wa kutoa msaada huo.”
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.