Home Soka Ninja Arudi Zenji

Ninja Arudi Zenji

by Dennis Msotwa
0 comments

Aliyekuwa mlinzi wa Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ amerejea visiwani Zanzibar baada ya klabu ya LA Galaxy kusitisha mkataba wake imefahamika

Aidha Wakala wa mchezaji huyo amesema pia klabu ya MFK Karvina ya Jamhuri ya Czech ambayo ndio ilimsajili Ninja na baadae kumtoa kwa mkopo LA Galaxy, nayo imesitisha mkataba wake bila kutoa sababu zozote

Ninja alirejea nchini baada ya ligi kuu ya Marekani kumalizika na alitakiwa kurudi huko Marekani mwezi huu

banner

Inaelezwa kwa sasa anafuatilia kibali cha kurudi Ulaya kwenda kufanya majaribio katika timu nyingine ambazo zimeonyesha kuhitaji huduma yake

Ninja aliitumikia klabu ya Yanga kwa misimu miwili kabla ya kugoma kuongeza mkataba mwezi Julai baada ya kupata ofa ya kujiunga na MFK Karvina

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited