Pengine ni kinyume na watu walivyokua wanafikiri kuwa kocha Juma Pondamali alitimuliwa katika klabu ya Yanga sc lakini kocha huyo ameamua kufunguka ukweli juu ya kuondoka kwake.
Kocha huyo mwenye mbwembwe na mpenzi wa mziki wa dansi alisema kuwa hakufukuzwa klabuni hapo bali yeye mwenyewe aliomba kuondoka baada ya kuongea na mwenyekiti wa klabu hiyo Dk.Mshindo Msolla ambapo alimfungika mipango ya timu hiyo kwa msimu huu nan ndipo aliomba kuondoka ili apate stahiki zake.
“Baada ya kukubaliana na Msolla niliamua niondoke ili nipate stahiki zangu kwa maana nilifahamu timu haiwezi kufikia malengo yake na benchi la ufundi lingetimuliwa kabla ya msimu kuisha jambo ambalo lilitokea baadae”.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.