Home Soka Rasmi Simba vs Yanga

Rasmi Simba vs Yanga

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc itakutana na Yanga sc katika hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho baada ya kufanikiwa kuifunga Azam fc mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam.

Simba sc walitawala mchezo na kufanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia kwa Nahodha John Boko dakika ya 40 akifunga kwa kichwa kupitia pasi ya juu ya Francis Kahata Nyambura bao lililodumu hadi mapumziko.

Iliwachukua Simba sc dakika 10 za kipimdi cha pili kuandika bao la pili kupitia kwa Mwamba wa Lusaka Cletous Chama aliyefunga bao zuri kupitia pasi ya Shomari Kapombe.

banner

Matokea hayo yanamaanisha kuwa Simba sc itakutana na Yanga sc ambayo ilimfunga Kagera Sugar kwa mabao 2-1 huku nusu fainali nyingine ni Namungo Fc dhidi ya Sahare All Stars.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited