Kocha mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amefurahishwa na kiwango cha mchezaji wake mpya Saido Ntibazonkiza alichokionyesha katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida United.
Kaze aliyemsajili mchezaji huyo ukiwa na usajili wake wa kwanza amesema kiwango alichokionyesha mchezaji wake anakifurahia kwani ameongeza kitu katika timu yake.
“Saido ni mchezaji mzuri na ameongeza kitu kwenye kikosi, ni mchezaji kiongozi na ameongoza vyema wachezaji wenzake”.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Saido alicheza mchezo wake wa kwanza katika mchezo huo na kufanikiwa kufunga mabao mawili huku akitoa pasi za kufunga zaidi ya tano lakini umakini mdogo wa Waziri Junior na Ditram Nchimbi ulisababisha kukosa mabao ya wazi.