Home Soka Saido Amfurahisha Kaze

Saido Amfurahisha Kaze

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amefurahishwa na kiwango cha mchezaji wake mpya Saido Ntibazonkiza alichokionyesha katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida United.

Kaze aliyemsajili mchezaji huyo ukiwa na usajili wake wa kwanza amesema kiwango alichokionyesha mchezaji wake anakifurahia kwani ameongeza kitu katika timu yake.

“Saido ni mchezaji mzuri na ameongeza kitu kwenye kikosi, ni mchezaji kiongozi na ameongoza vyema wachezaji wenzake”.

banner

Saido alicheza mchezo wake wa kwanza katika mchezo huo na kufanikiwa kufunga mabao mawili huku akitoa pasi za kufunga zaidi ya tano lakini umakini mdogo wa Waziri Junior na Ditram Nchimbi ulisababisha kukosa mabao ya wazi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited