Home Soka Samata,Msuva Kuwakosa Malawi

Samata,Msuva Kuwakosa Malawi

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wa timu ya Taifa ya Tanzania(Taifa Stars) Mbwana Samata na Saimon Msuva wataukosa mchezo wa kirafiki wa timu hiyo dhidi ya Malawi utakaofanyika siku ya Jumapili kutokana na Sababu mbalimbali.

Wakati Msuva atakuwa na klabu yake [Wydad Casablanca] kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Kaizer Chiefs upande wa Samata yeye atakua na udhuru kutokana na matatizo ya kifamilia yanayomkabili.

Kwa Upande wa meneja wa timu Nadir Haroub Canavaro alisisitiza kuwakosa wachezaji hao huku akisema kuwa maandalizi yanaendelea ”Maandalizi yanaendea, leo kutakuwa na mazoezi asubuhi kwenye uwanja wa Taifa. Kila mchezaji anatamani kucheza mechi ya Jumapili [Tanzania vs Malawi] lakini benchi la ufundi ndio litaamua nani atapata nafasi kwenye mchezo huo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited