Winga wa kimataifa wa England Jadon Sancho amejiunga rasmi na mashetani wekundu manchester united akitokea Borussia Dortmund ya Ujerumani kwa ada ya paundi milioni 77 za Kiingereza.
Sancho amesaini mkataba wa miaka mitano hadi 2026 wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi’.
Mchezaji huyo ametambulishwa hivi leo katika viunga vya Carringhton jijini Manchester akikabidhiwa jezi namba 25 mara baada ya kukamlika kusainiwa nyaraka kadhaa zilizokuwa zimebakia.
Usajili huo umeshusha presha kwa mashabiki wa man utd waliokuwa na hofu ya kusajiliwa kwake hasa baada ya kuhusishwa kwa muda mrefu.