Home Soka Senzo CEO mpya Yanga SC

Senzo CEO mpya Yanga SC

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Yanga imemtangaza rasmi Bw Senzo Mbatha Masingiza kuwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.

Kuteuliwa kwa Senzo katika nafasi hiyo mpya ndani ya Yanga kunatokana na utekelezwaji wa mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo na anakuwa ni mtu wa kwanza katika historia ya klabu hiyo.

Senzo raia wa Afrika ya Kusini kabla ya kuwa kaimu mtendaji mkuu alikuwa akihudumu katika klabu hiyo kama mshauri hasa kuelekea katika mfumo wa mabadiliko,hivyo cheo chake hiko kipya sasa kitamfanya awe na nguvu ya kiutendaji katika kuhakikisha Yanga inapiga hatua kubwa katika kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya timu hiyo.

banner

Mbatha aliwahi kuhudumu nafasi ya CEO katika klabu ya soka ya Simba kabla ya kuachana nayo na kutua kwa Wananchi ambako amepatiwa cheo hicho kikubwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited