20

Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na michezo imesema kuwa ilifanya kikao na TFF, TPLB, Serikali, BMT, Simba na Yanga kuhusu hatma ya mchezo wa Simba na Yanga baada ya Kikao hicho kwa pamoja wamekubaliana yafuatayo.
1-Mchezo huo wa Simba na Yanga urudiwe kuchezwa hivyo TPLB na TFF wapange tarehe ya kuchezwa mchezo huo.
2-Kuuhusu fedha ya mashabiki waliolipa Wizara imeagiza kituo cha kitaifa cha data (Data center) kuwajeshea tiketi mashabiki wote 43,947 walikuwa wamekata tiketi zao na watumie ticket hizo kuangalia mchezo huo.
3-Mashabiki wengine ambao walikuwa hawajakata tiketi wataruhusiwa kukata tiketi zilizobaki kuhusu uwezo wa uwanja wa Benjamin Mkapa.


4-Pia Waziri ameahidi kuitisha Kikao haraka kati ya TFF na Yanga ili kumaliza tofauti zao.