Klabu ya Simba sc imezindua applications ya mtandao inayosaidia upatikanaji wa taarifa mbalimbali za klabu hiyo huku kila mwanachama atakaejiunga atachangia kiasi cha shilingi elfu mbili kwa mwezi.
Applications hiyo itajulikana kama Simba App na inapatikana kwa njia zote za mifumo ya simu yaani AppStore na Playstore huku ikitarajiwa kuingiza mapato ya kutosha kwa klabu hiyo kutokana na kurahisisha upatikanaji wa taarifa muhimu za klabu.
Aidha wazo la klabu za ligi kuu nchini kuwa na huduma hiyo ilizinduliwa na Dismas Ten aliyekua afisa habari wa klabu ya Yanga sc ambapo akiwa katika klabu ya Mbeya City alianzisha wazo hilo na alilileta Yanga sc ambao kwa msimu uliopita waliingiza takribani milioni 240 za kitanzania.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.