Home Soka Simba sc Yaahirisha Uzinduzi wa Jezi

Simba sc Yaahirisha Uzinduzi wa Jezi

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba sc imeahirisha tukio la uzinduzi wa jezi mpya za msimu wa 2021/2022 lililokua limepangwa kufanyika leo Septemba 4 jijini Dar es salaam huku matukio yote yakiwekwa pamoja katika maadhimisho ya wiki ya Simba sc kuanzia Septemba 13.

Awali klabu hiyo ilipanga kuzindua rasmi jezi hizo lakini jana ilitangaza kuanza kuziuza rasmi madukani baada ya jezi hizo kuvuja na kufanya mashabiki kuongeza presha kwa msambazaji aliyeamua kuuza kabla ya uzinduzi rasmi wa jezi hizo mapema hii leo.

banner

Klabu hiyo imetoa Tangazo rasmi la kuahirisha uzinduzi huo masaa machache yaliyopita kupitia mitanda yake ya kijamii japo maamuzi hayo yalitegemewa na mashabiki wengi kutokana na hali halisi iliyojitokeza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited