Home Soka Simba sc Yafuzu Kibabe

Simba sc Yafuzu Kibabe

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba sc imefuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika baada ya kuitandika Fc Platnum ya Zimbabwe kwa mabao 4-0 katika mchezo uliofanyika jijini Dar es salaam.

Platnum waliingia wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa awali walijikuta wakifanya faulo nyingi na kusababisha Simba sc kupata penati dakika ya iliyofungwa kiufundi na Erasto Nyoni dakika ya 38.

Dakika ya 61 kipindi cha pili shuti la Rally Bwallya lilipanguliwa na kipa wa Fc Platnum na kumkuta Shomari Kapombe aliyefunga bao la pili huku John Bocco na Cletous Chama wakifunga bao la tatu na nne dakika za 90 na 95.

banner

Simba sc inaingia katika hatua ya makundi ya klabu bingwa ikiwa na mara ya pili kwa miaka ya hivi karibuni baada ya kufanya hivyo msimu wa 2018/2019 ambapo ilitolewa hatua ya robo fainali na Tp Mazembe.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited