Home Soka Simba SC yaingia mkataba na ATCL

Simba SC yaingia mkataba na ATCL

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba imesaini mktaba wa miaka miwili na shirika la ndege nchini(ATCL) kushirikiana katika maswala mbalimbali ya usafiri pindi timu hiyo itakapokuwa inasafiri ndani na nje ya nchi.

Katika mkabana huo ATC ndio watakaokuwa na dhamana ya kuisafirisha Simba kwnye mashindano ya kimataifa,pia wanachama na mashabiki wa timu hiyo watanufaika kwa kupata nafasi ya kusafiri natimu hiyo.

Mtendaji Mkuu wa Simba SC Barbara Gonzalez amesema kuwa ”thamani ya mkataba huu ni zaidi ya milioni 400,wanachama na mashabiki wetu watapata tiketi za bure,watapata punguzo pamoja na kupewa kipaumbele pindi watakapokuwa na safari”.

banner

Naye Mkurugenzi  wa ATCL Injinia Ladislaus Matindi Simba watasaidia kuitangaza Air Tanzania kupitia safari zao katika mashindano ya kimataifa,pia timu ya wanawake ya Simba watavaa nembo ya Air Tanzania mbele ya jezi zao.Na upande wa Simba watapata fedha pamoja na faida nyingine.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited