Home Soka Spurs yamgeukia Nuno

Spurs yamgeukia Nuno

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Tottenham hotspurs ya Uingereza imeanza mazungumzo na kocha wa zamani wa klabu ya Wolves Mreno Nuno Espirito Santo. Hatua hiyo imekuja baada ya klabu hiyo kushindwa katika majaribio kadhaa ya kuwanasa makocha wakubwa duniani ambao hawakuvutiwa na mipango ya klabu hiyo.

Nuno hakuwa kwenye orodha ya awali ya makocha wanaohitajika na  Tottenham hadi alipowasili mkuruenzi mpya wa klabu hiyo Fabio Parattici ambaye ndiye aliempendekeza kuwa kocha mpya wa klabu hiyo ya kaskazini mwa London.

Nuno aliachana na klabu ya Wolves baada ya kumaliza kwa msimu wa ligi ya Uingereza 2020/2021 baada ya kuhudumu katika timu hiyo kwa miaka zaidi ya minne.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited