Home Soka Stars yangara ugenini kufuzu Qatar 2022

Stars yangara ugenini kufuzu Qatar 2022

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imepata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Benin ugenini katika harakati zake za kufuzu kombe la dunia 2022 nchini Qatar katika mchezo wa kundi J.

Simon Msuva aliipatia Tanzania bao pekee la mchezo dakika ya 6 kwa shuti kali lililotinga wavuni mara baada ya kuwachambua walinzi wa Benin katika dimba la

Stars sasa wamefikisha pointi saba katika michezo minne ya kundi hilo na kukaa kileleni kwa tofauti ya magoli ya kufunga kabla ya mchezo mwingine wa kundi hilo kati ya DR Congo na Madagascar.

banner

Kocha wa Taifa Stars alifanya mabadiliko kadhaa kwenye kikosi chake kwa kuwaanzisha mlinzi wa kati Kennedy Juma na mshambuliaji Kibu Denis wakichukua nafasi za John Bocco na Mzamiru Yassini.

Tanzania imebakiza michezo miwili pekee kwenye hatua za makundi dhidi ya DR Congo nyumbani na Madagascar ugenini na endapo watamaliza kinara wa kundi lao basi watasonga katika hatua inayofuata ya mtoano inayohusisha mataifa 10 yaliyomaliza kileleni mwa makundi yao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited