Home Soka Straika Mkongo Anukia Yanga sc

Straika Mkongo Anukia Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc ipo mbioni kukamilisha usajili wa mchezaji Glody Kilangalanga ambaye anaitumia klabu ya Bisha Fc inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Saudi Arabia baada ya kutorodhika na washambuliaji waliopo klabuni hapo.

Mpaka sasa jitihada zinafanyika kwa mabosi wa Yanga sc kumpata mshambuliaji huyo ama kwa kumsajili moja kwa moja na ikishindikana basi apatikane kwa mkopo kuja kuchukua nafasi ya Hafiz Konkoni ambaye mabosi hao hawajaridhishwa na uwezo wake wa kufumania nyavu mpaka sasa.

Bisha Fc bado ina mkataba na straika huyo ambaye ilimsajili kutoka Cs Cheba ya nchini Tunisia na mpaka sasa ndiyo inaleta ugumu katika kuinasa saini ya mshambuliaji huyo.

banner

Yanga sc awali ilikua na mpango wa kusajili Karamoko Sankara wa Asec Mimosa,Saimon Msuva ama Ranga Chivaviro sajili ambazo zilikwama kutokana na sababu mbalimbali.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited