Home Soka Straika Rasta Kutua Yanga

Straika Rasta Kutua Yanga

by Sports Leo
0 comments

Alfred Raul ambaye ni wakala wa mshambuliaji wa kimataifa wa Burkina Faso, Yacouba Sogne amethibitisha kuwa Nyota huyo wa zamani wa Asante Kotoko ya Ghana atajiunga na Klabu ya Yanga SC ifikapo mwisho wa msimu huu.

Wakala huyo anayeishi nchini Ufaransa amesema tayari mazungumzo yalishafanyika na nyota huyo alishakubali kutua Yanga kinachosubili tu ni mipaka ya Burkina Faso ifunguliwe ili aweze kuja nchini kusaini mkataba.

Hata hivyo kocha wa zamani wa klabu ya Yanga Hans Van De Plujm amesema staa huyo ni mchezaji mzuri japo thamani yake halisi sio hiyo inayotajwa kwani inakuzwa na mitandao na ana uwezo wa kuitafutia klabu hiyo mastaa wa maana kwa bei chee.

banner

Yanga imekua ikihangaika kupata mshambuliaji baada ya waliokuwapo kushindwa kuendana na kasi ya timu hiyo na hivyo kuna uwezekano mkubwa watatemwa muda wowote.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited