Home Soka Takukuru Yachunguza Mamilioni Tff

Takukuru Yachunguza Mamilioni Tff

by Sports Leo
0 comments

Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) yawasiliana na CAF kuchunguza ushiriki wa rais wa shirikisho la soka Tanzania TFF Wallace Karia katika kashfa ya ubadhirifu wa fedha za CAF baada ya FIFA kumfungia rais wa CAF Ahmad Ahmad kutojihusisha na masuala ya soka kwa miaka 5 kutokana na kashfa ya ubadhirifu.

Inadaiwa Wallace Karia ni miongoni mwa wanufaika kwa kupata mgao wa dola 20,000 kutoka Caf ambazo zilikua kwa ajili ya matumizi ya Rais wa Shirikisho kwa mujibu wa Caf.

Akijibu kuhusu suala hilo Brig. Jen. John Mbungo,Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru alisema”Tumewasiliana na CAF, tumeanza uchunguzi, unajua hili suala ni jipya na ndio kwanza tumeanza uchunguzi, siwezi kuahidi itachukua muda gani, lazima kila hatua izingatiwe kwenye uchunguzi huu ili kama Wallace Karia amehusika na wote walionufaika na ubadhirifu huo waweze kubainika na kuchukuliwa hatua za kisheria”

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited