Home Soka Tambwe Anukia Jangwani

Tambwe Anukia Jangwani

by Sports Leo
0 comments

Inasemekana uongozi wa klabu ya Yanga sc upo kwenye mipango ya kumsajili mshambuliaji Amis Tambwe kwa mkataba wa muda mfupi ili kuongeza nguvu katika kikosi cha timu katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.

ambwe kinara wa mabao wa muda wote kwa wachezaji wa kigeni ligi kuu ya Tanzania, anaweza kurejea kuitumikia Yanga mpaka mwishoni mwa msimu

Yanga inahitaji kuboresha safu yake ya ushambuliaji baada ya kuachana na washambuliaji Sadney Urikhob na Juma Balinya

banner

Wachezaji hao walishindwa kutamba licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki

Msimu uliopita Tambwe aliifungia Yanga mabao nane licha ya kutopata nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza mara kwa mara

Hakuna shaka anaweza kuongeza kitu kwenye safu ya ushambuliaji ambayo kwa sasa inamtegemea David Molinga pekee

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited