Inasemekana uongozi wa klabu ya Yanga sc upo kwenye mipango ya kumsajili mshambuliaji Amis Tambwe kwa mkataba wa muda mfupi ili kuongeza nguvu katika kikosi cha timu katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
ambwe kinara wa mabao wa muda wote kwa wachezaji wa kigeni ligi kuu ya Tanzania, anaweza kurejea kuitumikia Yanga mpaka mwishoni mwa msimu
Yanga inahitaji kuboresha safu yake ya ushambuliaji baada ya kuachana na washambuliaji Sadney Urikhob na Juma Balinya
Wachezaji hao walishindwa kutamba licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki
Msimu uliopita Tambwe aliifungia Yanga mabao nane licha ya kutopata nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza mara kwa mara
Hakuna shaka anaweza kuongeza kitu kwenye safu ya ushambuliaji ambayo kwa sasa inamtegemea David Molinga pekee