Mbunge wa Kinondoni, Abbas Tarimba ameishauri Serikali kuweka sharti la kila kampuni ya michezo ya kubahatisha [Betting] kudhamini timu ya michezo kama sharti la kupewa leseni ikiwa ni njia ya kurudisha kwa jamii.
Tarimba ambaye alikua meneja oparesheni wa kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Sportspesa ameahidi kulipeleka suala hilo Bungeni kama hoja binafsi ili liweze kufanyiwa kazi na mamlaka husika.
Endapo wazo hilo litafanyiwa kazi na kupitisha litasaidia kupunguza makali ya kuendesha klabu ambayo timu hukutana nazo kutokana na kuwa na uchache wa vyanzo vya mapato.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.