Home Soka Tarimba Alia na Michezo ya Kubahatisha

Tarimba Alia na Michezo ya Kubahatisha

by Dennis Msotwa
0 comments

Mbunge wa Kinondoni, Abbas Tarimba ameishauri Serikali kuweka sharti la kila kampuni ya michezo ya kubahatisha [Betting] kudhamini timu ya michezo kama sharti la kupewa leseni ikiwa ni njia ya kurudisha kwa jamii.

Tarimba ambaye alikua meneja oparesheni wa kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Sportspesa ameahidi kulipeleka suala hilo Bungeni kama hoja binafsi ili liweze kufanyiwa kazi na mamlaka husika.

Endapo wazo hilo litafanyiwa kazi na kupitisha litasaidia kupunguza makali ya kuendesha klabu ambayo timu hukutana nazo kutokana na kuwa na uchache wa vyanzo vya mapato.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited