Home Soka Tetesi za soka leo Jumamosi

Tetesi za soka leo Jumamosi

by Sports Leo
0 comments

Tottenham Hotspur wanataka kumsajili winga hatari wa Wolverhampton Adama Traore katika dirisha dogo la uasjili mwezi Januari.(Fabrizio Romano)

Chelsea watatakiwa kumpa mkataba mnono mlinzi wa kati Antonio Rudiger ili kusaini mkataba mpya,vinginevyo ataondoka bure mwishoni mwa msimu huu.(Football Insider)

Real Madrid wana mpango wa kuwasajili kwa pamoja washambuliaji wawili hatari duniani Kylian Mbappe wa PSG na Erling Haaland wa Dortmund katika dirisha la usajili la majira ya joto.(ESPN)

banner

Newcastle United wapo karibu kufikia makubaliano na mabingwa wa Hispania Atletico Madrid ili kumsajili mlinzi wa kulia Kieran Trippier.(The Athletic)

Tottenham wanataka kumsajili bure kiungo mshambuliaji wa FC Barcelona Philipe Coutinho lakini klabu yake wanataka paundi milioni 17 ili kumwachia.(El Nacional)

Manchester United wapo tayari kulipa ada ya paundi milioni 16 ili kununua mkataba wa mshambuliaji Julian Alvarez wa River Plate ya Argentina anayetajwa kuwa Tevez mpya huko kwao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited