Thiago Silva amesema yu tayari kusalia katika mojawapo ya klabu za bara Ulaya kwa misimu miwili zaidi baada ya waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kumweleza kwamba hawatarefusha mkataba wake mwishoni mwa muhula huu.
Psg kupitia kwa mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Leonardo walithibitisha kuwa hawatamuongeza mkataba nahodha huyo wa muda mrefu klabuni hapo.
Taarifa za awali zinadai kwamba klabu ya Arsenal ipo mbioni kumsajili staa huyu mwenye miaka 35 japo watakumbana na upinzani mkali kutoka Ac Milan,Everton,Wolves na Westham huku pia timu za kutoka Marekani,Qatar na Brazil zinammndea staa huyo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.