Home Soka Uchebe Asimamishwa Simba

Uchebe Asimamishwa Simba

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Simba sc imemsimamisha kazi kocha mkuu Patrick Aussems mpaka Novemba 28 mwezi huu ambapo kikao cha bodi ya wakurugenzi kitakapokaa na kutoa maamuzi.

Kwa mujibu wa ripoti za ndani zinadai chanzo cha kusimamishwa kazi kocha huyo ni kutokana na kutohudhuria kikao cha kujieleza baada ya kuwa amesafiri ghafla kwenda nje ya nchi alikodai ana matatizo binafsi.

Uongozi wa Simba ulichukizwa na kutohudhuria kwa kocha huyo katika kikao hicho kilichopangwa kufanyika katika ofisi ya mtendaji mkuu wa klabu hiyo Senzo Masingisa zilizopo katikati ya jiji bila ya kutoa taarifa zozote.

banner

Aussems amethibitisha kupokea barua hiyo huku akisema anawasiliana na wanasheria wake waliopo ulaya ili kujua nini cha kufanya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited