Home Soka Ulimwengu Matatani Drc

Ulimwengu Matatani Drc

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa timu ya Tp Mazembe  Thomas Ulimwengu ameshukiwa na kocha wa timu hiyo Mihayo Kazembe kutokana na kushuka kiwango katika michezo kadhaa ya timu hiyo tofauti na msimu uliopita ambapo alikua moto wa kuotea mbali.

Kazembe anasema licha ya kumpa nafasi mara nyingi mshambuliaji huyo lakini anakosa umakini kwa kiasi kikubwa hivyo anafikiri kutafuta mbadala wake kwa ajili ya kuongeza makali kikosini humo.

Ulimwengu licha ya kucheza katika klabu hiyo katika michuano ya kimataifa amekosa nafasi katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kutokana na kocha Kim Poulsen kutoridhishwa na kiwango chake.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited