Home Soka Yanga sc Inatisha,Mukoko Atupia 2

Yanga sc Inatisha,Mukoko Atupia 2

by Sports Leo
0 comments

Yanga sc bado ya moto baada ya jana kuifunga klabu ya Mbuni Fc inayoshiriki ligi ya daraja la kwanza yenye maskani yake jijini Arusha katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mchezo ambao Yanga sc ililenga kuwaongezea utimamu wa mechi mastaa wake wasiopata nafasi ya kuanza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza ambapo wachezaji kama Erick Johora,Paul Godfrey,Mukoko Tonombe,Chrispine Ngushi,Balama Mapiduzi na wengineo wakianza mchezo huo.

Yanga sc ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ambayo yalipatakana kwa penati ambazo zote zilifungwa kiufundi na kiungo Mukoko Tonombe aliyecheza kama mlinzi wa kati sambamba na Ibrahim Bacca aliyesajiliwa hivu karibuni kutoka KmKm ya Zanzibar baada ya kufanya vizuri katika michuano ya kombe la mapinduzi.

banner

Pia kivutio kikubwa kwa mashabiki wa soka hapo uwanjani ni pale alipoingia winga Chico Ushindi ambaye alichukua nafasi ya Deus Kaseke dakika ya 64 na kusababisha shangwe kwa mashabiki huku wakikoshwa na kiwango cha staa katika kuwalaghai mabeki.

Yanga sc imesalia jijini Arusha ikiendelea na maandalizi ya mechi dhidi ya Polisi Tanzania itakayochezwa siku ya jumapili Januari 23 katika uwanja wa ushirika mjini Moshi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited