Home Soka Yanga SC yaanza vibaya klabu bingwa

Yanga SC yaanza vibaya klabu bingwa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Yanga imeanza vibaya michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kupoteza kwa goli 1-0 nyumbani dhidi ya Rivers United ya Nigeria katika mchezo wa kwanza wa hatua za awali za mtoano.

Yanga ilianza mchezo huo kwa kasi wakionesha kuhitaji matokeo ya haraka kwa kutengeneza nafasi ambazo hata hivyo hawakuweza kuzitumia vizuri.

Kipindi cha upepo ulibadilika ambapo safari hii ni Rivers ndio waliutawala zaidi mchezo na kufanikiwa kupata goli pekee la mchezo dakika ya 51 kupitia kwa mshambuliaji Moses Omodumuke aliyeunganisha kwa kichwa baada ya mabeki wa Yanga kuzubaa.

banner

Yanga sasa ina mlima mkubwa wa kupanda kupindua matokeo katika mchezo wa marudiano utakaofanyika wiki ijayo nchini NIgeria.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited