Home Soka Yanga Yapoteza Pointi

Yanga Yapoteza Pointi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga imeshindwa kuendelea kupunguza pengo la pointi dhidi ya mahasimu wao Simba baada ya kukubali sare ya 1-1 dhidi ya Mbeya city katika mchezo uliofanyika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Mbeya city walliokuwa wakicheza kwa mkakati maalumu wa kutofunguka walifanikiwa kupata bao dakika ya 42 baada ya beki Lamine Moro kujifunga katika harakati za kuokoa mpira.

Morrison aliendelea kuwa shujaa wa Yanga baada ya kufunga bao la kusawazisha dakika ya 75 na kufanikiwa kurejesha pointi moja iliwafanya kufikisha pointi 38.

banner

Yanga inakumbukumbu ya kushinda bao 1-0 mbele ya Ruvu Shooting na Mbeya City ilishinda bao 1-0 mbele ya Tanzania Prisons.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited