Home Soka Yanga Yashtuka Janja ya Morisson

Yanga Yashtuka Janja ya Morisson

by Sports Leo
0 comments

UONGOZI wa Yanga umesema kuwa kiungo wao Mghana, Bernard Morrison asitegemee wao kutangaza kuvunja mkataba wake huku wakisisitiza kuwa mchezaji huyo bado ni mali yao mwenye mkataba wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea wa Yanga. 

Hiyo ikiwa ni siku chache tangu Mghana huyo kuondoka uwanjani wakati timu hiyo ikiendelea na mchezo wake wa Nusu Fainali ya Kombe la FA walipocheza na Simba na kulala kwa mabao 4-1, baada ya kutolewe katika dakika ya 66 na Ditram Nchimbi kuingia kuchukua nafasi yake.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata na kuthibitishwa na Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela, kiungo huyo bado ni mali yao hadi Julai 15, 2022, baada ya kuongeza mkataba wake wa miaka miwili.

Mwakalebela alisema kuwa kiungo huyo kama anafanya matukio ya kiutovu wa nidhamu kwa makusudi akitegemea uongozi utasitisha mkataba wake na kuondoka kama mchezaji huru, basi imekula kwake.

Cc:Champion na Mitandao

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited