Home Soka Yanga Yatua Usiku

Yanga Yatua Usiku

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya soka ya Yanga sc imewasili usiku wa leo kutoka nchini Botswana ilipokua imeenda kukipiga na Township Rollers mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa 1-0.

Timu hiyo ambao ni mabingwa mara 27 wa ligi kuu Tanzania bara wametua nchini saa saba usiku na kulakiwa na mashabiki wa timu hiyo ambao walijitokeza kuwapokea baada  ya kuwa wamefanikiwa kufuzu kwende raundi ya kwanza ya michuano hiyo ambapo watakutana na Zesco united ya Zambia.

Baada ya kutua timu hiyo iliunganisha kambini katika hotel ya Nefaland iliyopo Manzese jijini Dar es salaam ili kujiandaa na mchezo dhidi ya Ruvu shooting utakaopigwa siku ya jumatano.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited