Home Soka Yondani Awatega Vigogo Yanga sc

Yondani Awatega Vigogo Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Viongozi wa Yanga wapo mtegoni kufuatia ripoti ya kocha Luc Eymael kumtaja Kelvin Yondani katika orodha ya mastaa ambao anaweza kuwatema ili kusajili vifaa vipya klabuni hapo.

Licha ya ripoti hiyo kuonyesha hivyo taarifa za ndani kutoka katika kamati ya usajili ya klabu hiyo zinadai baadhi ya wajumbe wameonyesha kutokubaliana na uamuzi huo kutokana na ukongwe wa staa huyo klabuni hapo.

Pia imetajwa kitendo cha kumuacha beki huyo ni kurudia makosa yaliyofanywa na klabu ya Azam fc ambayo iliachana na wakongwe na kuwauzia silaha wapinzani wao Simba sc ambao waliwasajili na kufanikiwa kuchukua ubingwa mara mbili mfululizo.

banner

Tayari beki huyo ameshafahamu mpango huo wa kumtema na ameshaanza kuangalia malisho mengine huku Simba ikiwa kipaumbele chake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited