Viongozi wa Yanga wapo mtegoni kufuatia ripoti ya kocha Luc Eymael kumtaja Kelvin Yondani katika orodha ya mastaa ambao anaweza kuwatema ili kusajili vifaa vipya klabuni hapo.
Licha ya ripoti hiyo kuonyesha hivyo taarifa za ndani kutoka katika kamati ya usajili ya klabu hiyo zinadai baadhi ya wajumbe wameonyesha kutokubaliana na uamuzi huo kutokana na ukongwe wa staa huyo klabuni hapo.
Pia imetajwa kitendo cha kumuacha beki huyo ni kurudia makosa yaliyofanywa na klabu ya Azam fc ambayo iliachana na wakongwe na kuwauzia silaha wapinzani wao Simba sc ambao waliwasajili na kufanikiwa kuchukua ubingwa mara mbili mfululizo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Tayari beki huyo ameshafahamu mpango huo wa kumtema na ameshaanza kuangalia malisho mengine huku Simba ikiwa kipaumbele chake.