Home Makala Yanga sc Watua Dodoma Kibabe

Yanga sc Watua Dodoma Kibabe

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha klabu ya Yanga sc kimewasili jijini Dodoma kuelekea mchezo wa ligi kuu ya Nbc dhidi ya Dodoma jiji siku ya Jumapili utakaofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini humo.

Yanga sc itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kuwafunga walima zabibu hao kwa magoli 4-1 katika mchezo wa awali jijini Dar es salaam ambapo pia watahitaji kuongeza alama katika mbio za ubingwa wa ligi hiyo.

Yanga sc imefikisha jumla ya michezo mitatu bila ushindi japo imeendelea kukaa kileleni ikiwa na alama 57 katika michezo 23 huku presha ya ubingwa ikitajwa kama chanzo cha kupata matokeo hayo.

banner

Mchezo huo awali ulikua uchezwe saa moja usiku lakini kutokana na uwanja kuwa na matumizi mengine hivi sasa utachezwa saa 1o jioni katika uwanja huo huo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited