by Sports Leo
0 comments

klabu ya Simba itamkosa Mlinda mlango Aishi Salum Manula ambaye alipata majeraha kwenye vidole vya mikono mwishoni mwa wiki iliyopita kabla ya mchezo dhidi ya Geita Gold baada ya kuangukiwa na kioo kilimkata  kidole cha mkono.

Beno Kakolanya ambaye amekaa langoni kwenye michezo yote ya Simba kwenye michuano hii msimu huu ataendelea na jukumu hilo kwenye mchezo wa leo dhidi ya watani wao Yanga sc utakaoanza mapema hivi leo.

Aidha Simba ambaye ni bingwa mtetezi wa michuano hii atawakosa baadhi ya wachezaji wengine kama vile Hassan Dilunga,Clatous Chama,Jonas Mkude kutokana na kutokua fiti hasa baada ya kuwa na majeraha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited