Home Makala Simba sc Yatua kwa Mmorroco wa Apr

Simba sc Yatua kwa Mmorroco wa Apr

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc ipo katika mazungumzo na kocha Adil Erradi raia wa Morroco kwenda kuchukua nafasi ya kocha Pablo Franco ambaye wamemtimua klabuni hapo hivi leo.

Kocha huyo ambaye kwa sasa ni kocha wa klabu ya APR ya nchini Rwanda tayari yupo nchini toka juzi akijadiliana na mabosi wa klabu hiyo kuhusu kusaini mkataba huku akiaga nchini Rwanda kwa mapumziko mafupi.

Simba sc inahitaji kocha mpya baada ya kumtimua Pablo kwa kigezo cha kutofika malengo yaliyopo katika mkataba wake aliousaini wakati akiwa anawasili klabuni hapo akitakiwa kuifikisha timu hiyo nusu fainali ya michuano ya kimataifa na kuchukua makombe mawili ya ligi kuu na kombe la shirikisho la Azam ambapo mpaka sasa kote huko ameshindwa kufanikisha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited