Home Makala Manzoki,Lwanga Kuwavaa Yanga sc

Manzoki,Lwanga Kuwavaa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc kesho inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Vipers Fc katika kuadhimisha tamasha la wiki ya mwananchi ambalo hufanyika kila mwaka mwanzoni mwa msimu mpya wa ligi kuu nchini.

Katika Tamasha la mwaka huu Yanga sc itamenyana na mabingwa wa ligi kuu nchini Uganda Vipers Fc ambao wamekuja na mshambuliaji anayewaniwa na klabu ya Simba sc Cezar Manzoki mfungaji bora na mchezaji bora wa ligi ya Uganda msimu uliopita.

Mbali na Manzoki ambaye klabu yake imewataka Simba sc kama wanamhitaji kupeleka ofa yao mezani wakigoma na kukanusha kuwa anakaribia kumaliza mkataba wake pia Thaddeo Lwanga ambaye ametemwa na Simba sc amejiunga na klabu hiyo na atashiriki mchezo huo hapo kesho.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited