Home Makala Mapro 12 sasa Ruksa

Mapro 12 sasa Ruksa

by Sports Leo
0 comments

Bodi ya ligi kuu nchini (TPLB) imetangaza mabadiliko ya kanuni za usajili wa wachezaji wa kigeni ambapo klabu sasa zinaruhusiwa kusajili wachezaji 12 wa kigeni huku wakiruhisiwa kuwatumia wote katika mchezo mmoja tofauti na awali ambapo walikua wanaruhusiwa wachezaji 8 pekee.

Mabadiliko hayo yamekuja baada ya kikao na wadau wa ligi kuu wakiwemo viongozi wa klabu zote za ligi kuu nchini ambapo klabu zilikubali mapendekezo hayo.

Klabu za Simba sc,Yanga sc na Azam Fc ndio wafaidikaji wakubwa wa mabadiliko hayo kwa wana wachezaji wengi wa kigeni kiasi kuna kipindi kanuni ilikua inawabana katika uchaguzi wa kikosi na kufanya baadhi ya mastaa kukaa jukwaani licha ya kusajiliwa kwa pesa nyingi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited