Mwamuzi wa Kimataifa wa Tanzania ,Ramadhan Kayoko Ndiye atakayechezesha Derby ya Kariakoo kati ya Yanga na Simba ambayo inatarajia kufanyika Jumapili ya wiki hii kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Oktoba 23.
Kayoko amekua na uzoefu wa kuchezesha michezo hiyo akiwa ameshazesha mara kadhaa pasi kuzua malalamiko makubwa tofauti na wenzake mabao mara kadhaa wameshindwa kuhimili presha ya mchezo huo.
Refa huyo atasaidiwa na Ramadhani Mkono kutoka Tanga na Janeth Balama kutoka Iringa huku Mwamuzi wa akiba akiwa ni Elly Sasii kutoka Dar es salaam ambapo waamuzi hao kwa pamoja ndio watakaoamua hatma ya wababe hao wa ligi kuu nchini nani akae kileleni baada ya dakika tisini za mchezo huo ambao Yanga sc ndio watakua wenyeji.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.