Home Makala Yanga sc Yahamia Chamazi Complex

Yanga sc Yahamia Chamazi Complex

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc sasa itatumia uwanja wa Chamazi Complex kama uwanja wa nyumbani katika mchezo wa kombe la shirikisho la AzamTv baada ya uwanja wa Benjamin Mkapa kuwa katika matengenezo kwa muda.

Yanga sc itautumia uwanja huo unaomilikiwa na klabu ya Azam Fc katika mchezo wa siku ya ijumaa dhidi ya Tanzania Prisons mchezo wa hatua ya mtoano ya kombe la shirikisho unaotarajiwa kuanza majira ya saa moja usiku.

Pamoja na hayo bado klabu ya Yanga sc itaendelea kuutumia uwanja wa Benjamini Mkapa kama uwanja wa nyumbani katika michuano ya kimataifa dhidi ya Real Bamako utakaofanyika siku ya Jumatano march 8.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited