Mchezo wa ligi kuu nchini kati ya Singida Big Stars na Coastal Union ya mkoani Tanga umemalizika katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga bila mbabe baada ya kutoka sare ya 1-1 baina ya timu hizo.
Greyson Gerrad alianza kuipatia Coastal Union bao la mapema dakika ya 44 na kipindi cha pili Bright Adjei alipambana na kuisawazishia Singida Big Stars dakika ya 74 ya mchezo na kufanya mpaka filimbi ya mwisho inamalizika kwa sare ya 1-1.
Kutokana na matokeo hayo sasa Coastal Union wanakua katika nafasi ya 13 ya msimamo wa ligi kuu wakiwa na alama 26 huku Singida Big Stars wakiwa katika nafasi ya tatu na alama 49 huku timu hizo zikiwa zimecheza michezo 25 ya ligi kuu nchini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.