Home Makala Coastal,Singida Big Stars Hakuna Mbabe

Coastal,Singida Big Stars Hakuna Mbabe

by Dennis Msotwa
0 comments

Mchezo wa ligi kuu nchini kati ya Singida Big Stars na Coastal Union ya mkoani Tanga umemalizika katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga bila mbabe baada ya kutoka sare ya 1-1 baina ya timu hizo.

Greyson Gerrad alianza kuipatia Coastal Union bao la mapema dakika ya 44 na kipindi cha pili Bright Adjei alipambana na kuisawazishia Singida Big Stars dakika ya 74 ya mchezo na kufanya mpaka filimbi ya mwisho inamalizika kwa sare ya 1-1.

Kutokana na matokeo hayo sasa Coastal Union wanakua katika nafasi ya 13 ya msimamo wa ligi kuu wakiwa na alama 26 huku Singida Big Stars wakiwa katika nafasi ya tatu na alama 49 huku timu hizo zikiwa zimecheza michezo 25 ya ligi kuu nchini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited