Home Makala Saido Atemwa Burundi

Saido Atemwa Burundi

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha Mkuu wa Burundi ‘Intamba Mu Rugamba’, Etienne Ndayiragije amemwaacha nje ya kikosi kiungo wa Simba SC, Saido Ntibazonkiza wakati Burundi ikijiandaa kukabiliana na Namibia kwenye michezo ya kufuzu Afcon 2023 nchini Ivory Coast mwezi ujao.

Saido anatuhumiwa kwa utovu wa nidhamu baada ya kukataa kushiriki mchezo wa kirafiki dhidi ya Indonesia mapema mwezi Machi mwaka huu.

Mlinda mlango wa Coastal Union Justin Ndikumana ameitwa kikosini humo akiwa ni mchezaji pekee kutoka nchini kwa mastaa wanaocheza ligi kuu ya Nbc.

banner

Saido amekua na matatizo ya mara kwa mara ya kinidhamu ambapo hata alipokua na Yanga sc alitemwa katika kikosi hicho baada ya kukutwa na utovu wa nidhamu kuelekea mchezo wa nusu fainali ya kombe la shirikisho dhidi ya Simba sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited