Home Makala Katwila Aibukia Tanga

Katwila Aibukia Tanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Siku chache baada ya kuachana na Ihefu Sc Zuberi Katwila ameonekana akishirikiana na makocha wengine wa timu ya Taifa ya wanaume U15 katika kituo Cha ufundi Cha TFF, Mnyanjani, Tanga katika maandalizi ya mashindano ya CECAFA.

Ingawa haijafahamika bado kuhusu hatma yake baada ya kuchana na timu hiyo yenye makao yake Mbarali mkoani Mbeya tangu aachane nao rasmi siku ya Jumamosi huku pia kukiwa na taarifa za kujiunga na Singida Fountain Gate kama kocha msaidizi ama kurudi klabu yake ya zamani ya Mtibwa Sugar.

Katwila ameonekana kupitia video fupi iliyowekwa na mtandao wa kijamii wa shirikisho hilo inayoonekana hapo chini.

banner

Awali Katwila baada ya kuachana na Ihefu alisema kuwa mpaka sasa bado hajapata timu “Sijafanya mazungumzo na timu yoyote ila itakayokuwa tayari kunihitaji tukakubaliana mimi niko tayari hata Ihefu naweza kurudi kwa sababu sijaondoka kwa ubaya zaidi ya makubaliano,” Alisema Katwila

Kocha huyo alidumu klabuni hapo kwa miaka mitatu tangu alipojiunga na timu hiyo akitokea Mtibwa Sugar.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited