Home Soka Simba Sc Watua kwa Beki Coastal Union

Simba Sc Watua kwa Beki Coastal Union

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klab ya Simba Umefufua mpango wa kuipata saini ya mlinzi wa kati wa klabu ya Coastal Union Lameck Elias Lawi kuja kuongeza nguvu katika safu ya ulinzi ya klabu hiyo kusaidiana na Henock Inonga na Che Fondoh Malone.

Imefahamika kuwa ofa kutoka Simba Sc kwenda kwa wagosi wa kaya tayari imeshatumwa na kinachosubiriwa sasa ni majibu na makubaliano mengine ya kimkataba baina ya klabu hiyo pamoja na mchezaji mwenyewe.

Lawi ambaye ni beki bora chipukizi nchini kwa msimu uliopita ameonyesha nia ya kujiunga na Simba sc ambapo kutokana na kuwa na mkataba na Coastal hana budi kusubiri makubaliano baina ya klabu hizo yakamilike ndipo ajiunge na wekundi hao wa msimbazi.

banner

Simba sc ipo katika mpango kabambe wa kufanya maboresho makubwa katika kikosi chake ambacho kinasuasua kutokana na mastaa wa timu hiyo asilimia kubwa kuonekana kuchoka.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited