Home Soka Niyonzima Arudi Nyumbani

Niyonzima Arudi Nyumbani

by Sports Leo
0 comments

Hatimaye kiungo wa zamani wa Yanga sc na Simba sc Haruna Niyonzima amerudi nyumbani baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na klabu ya As Kigali ya nchini Rwanda.

Kiungo huyo mzaliwa wa Gisenyi nchini humo aliondoka nchini humo miaka kadhaa iliyopita na kuja nchini kujiunga na Yanga sc ambapo alijijengea ufalme baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa zaidi ya misimu mitano na kuamua kujiunga na wapinzani wao Simba sc alipokaa kwa miaka miwili tu.

Awali taarifa zilidai baada ya Simba sc kutoonesha nia ya kumuongezea mkataba kiungo huyo alitakiwa na klabu ya As Vita ya kongo.

banner

As kigali ni timu inayoshiriki ligi kuu nchini Rwanda na itashiriki michuano ya kombe la shirikisho mwakani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited