Home Makala Kaseke Atua Pamba Jiji

Kaseke Atua Pamba Jiji

by Sports Leo
0 comments

Winga wa zamani wa klabu ya Yanga sc na Singida Big Stars Deus Kaseke amejiunga na klabu ya Pamba Jiji Fc kwa mkataba wa miezi sita akiwa kama mchezaji huru.

Kaseke ambaye alikua hana timu tangu aachane na waajiri wake wa zamani ilikua ajiunge na Kengold Fc lakini dili hilo halikukamilika na sasa rasmi amejiunga na Pamba Jiji Fc yenye makao yake makuu jijini Mwanza.

Kocha Fred Felix Minziro ameamua kufanya maboresho katika kikosi hicho akisajili baadhi ya mastaa ili kuongeza nguvu katika kikosi hicho kueleka duru la pili la ligi kuu ya soka ya nbc.

banner

Kaseke ana uwezo wa kucheza nafasi zote za winga pamoja na kiungo mshambuliaji wa kati lakini pia akiweza kucheza kama beki wa kulia pale inapobidi.

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini Pamba Jiji ipo nafasi ya 12 ikiwa na alama 12 katika michezo 14 hivyo endapo itaendelea kufanya vibaya basi kukosa nafasi ya kushiriki ligi kuu msimu ujao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited