Home Soka As Vita Waitosa Siku Ya Mwananchi

As Vita Waitosa Siku Ya Mwananchi

by Sports Leo
0 comments

Timu ya As Vita ya nchini Kongo iliyokua ije nchini kumenyana na Yanga sc katika siku ya kilele cha tamasha la wiki ya mwananchi imeahirisha kuja nchini kucheza na wanajangwani hao kama ilivyoelezwa hapo awali.

Roul Shungu ambaye ni kocha msaidizi wa timu hiyo amethibitisha kuahirishwa kwa safari hiyo ya kuja nchini baada ya kutangazwa kwa ratiba ya michuano ya kombe la klabu bingwa barani Afrika ambapo timu hiyo itaanzia ugenini nchini Cameroon dhidi ya UMS de Loum.

Kwa mujibu wa ratiba ya tamasha hilo ilibidi timu hizo zimenyane Agusti 4 ambayo ndio siku ya kilele na timu hiyo ya Kongo ingebakiwa siku tano za maandalizi na kusafiri kwenda Cameroon kitu ambacho wakongo hao wameona ni vigumu ukizingatia umuhimu wa michuano hiyo.

banner

Pia kocha huyo amesisitiza ratiba hiyo ya Caf licha ya kuathiri ushiriki wao katika tamasha la wiki ya mwananchii pia itawalazimu kubadili ratiba yao ya maandalizi ya msimu ili kujiandaa na mechi hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited